Tunaweza sema mtu ana tatizo la shinikizo la damu pale ambapo msukumo wa damu ( blood pressure) huwa juu kwa muda mrefu, juu ya 140/90mmHg au chini ya hapo pale endapo mtu atakua anatumia dawa kwa ajili ya shinikizo la damu.
Shinikizo la damu hupitia hatua mbali mbali za awali kabla ya kuja kugundulika na tatizo hilo. Hatua zinaweza kuwa kama ifuatavyo:
Presha ya kawaida huwa chini ya 120/80mmHg.
Kidokezo cha presha kuanza kupanda (120-139)/(80-89)mmHg
Hatua ya kwanza ya shinikizo la damu (140-159)/(90-99)mmHg
Hatua ya pili ya shinikizo la damu 160/100mmHg au Zaidi
Mara nyingi dalili za shinikizo la damu huanza kujitokeza pale ambapo presha ya mwili ipo hatua ya kwanza juu ya 140/90mmHg, ndipo mtu huanza kujisikia uchovu usio na sababu ya msingi, kichwa kuuma, kifua kuuma, kupumua kwa shida,kukohoa, kizunguzungu, na dalili nyinginezo zinzoambatana na magonjwa ya moyo.
Shinikizo la damu ni moja kati ya magonjwa yasiyoambukizwa, ila kwa takwimu za shirika la afya la dunia ( WHO) linaonesha takribani watu zaidi ya bilioni moja duniani kote wanakabiliwa na tatizo hilo.
Hivyo, inashauriwa kuwa na mazoea ya kupima presha mara kwa mara ili kujua mapema endapo kutakua na viashiria vya shinikizo la damu na kuchukua hatua stahiki.
Kulingana na maendeleo ya kiteknolojia na kuongezeka kwa artificial food limekuwa tatizo kubwa ambalo limesababisha kuongezeka kwa idadi ya watu wenye high blood pressure
pia utumiaji wa vyakula vyenye mafuta mengi hasa fatty acid trigyceride yenye Omega3 ambayo ina kiwango kidogo cha protein asilima 1% ambapo lipid ni asimia 45% (LDLP) jamii inatakiwa kuepuka kutumia vyakula hivi ili kuepukana na tatizo la High Blood Pressure vyakula hivi ni pamoja na chips mayai na nyama ya nguruwe(rich in LDLP) vyakula hiv vinaweza kusababisha pia athreclerosis and cardiac attack
nashukuru sana Dr mkononi team kwa kazi nzuri maada hii nawaomba mjaribu kutoa maelezo ya kina kwa jamiii namna ya kupambana na tatizo hili na vyakula ambavyo mngeshauri jamii itumie na solution kama tatizo litatokea kwenye jamii
Tunashukuru sana bwana PASCAL MISILI kwa mchango wako mzuri na tutalifanyia kazi wazo lako. Endelea kutufuatilia.
Asante tupo pamoja blog hii inanipatia ujuzi mwingi sana barikiweni.
Nashukuru kwa mchango wako Dr Misili napenda kusisitiza ni hero kukinga kuliko kutibu tuepuke kula vyakula vynye mafuta Mara kwa mara